“Wanangu wapendwa! Leo maombi yangu pamoja nanyi ni kwa ajili ya amani. Mema na maovu yanapigana na kutaka kutawala duniani na katika mioyo ya watu. Muwe watu wa matumaini, maombi na imani kubwa kwa Mungu Muumba ambaye kwake yote yanawezekana. Wanangu, amani na itawale ndani yenu na karibu nanyi. Ninawabariki kwa baraka yangu ya kimama ili, wanangu, muwe furaha kwa wale wote mtakaokutana nao. Asanteni kwa kuitikia wito wangu. ”